Usiku wa kuamkia leo ulikuwa wa aina yake katika maeneo ya Leaders Club mara baada ya burudani kali kutoka kwa rapper wa Marekani T.I.
Akionekana mchangafu jukwaani mwanamuziki huyo alitumbuiza ngoma zake kali za kitambo na zile mpya kutoka kwa album yake mpya 'Paperwork' ambayo itaachiwa Jumanne hii tarehe 21.
T.I hata hivyo alichukua muda kuwaomba radhi mashabiki kwa kuchelewa kufika stejini na kuwalipa fadhila kwa performance hiyo ya aina yake katika usiku huo.
T.I alionekana pia kujibu watu wote walioongelea vibaya ziara yake ya kuja Africa na kusema yeye hajali watu wanaoizumgumzia vibaya Africa, na kuwachana kwa kibao cha 'Live Your Life'.
Kuelekea mwishoni, T.I alichukua picha ya pamoja na mashabiki "selfie" kama kuwashukuru kwa support walioionesha muda wote alivyokuwa akitumbuiza.
Licha ya T.I wasanii wengi kutoka Tanzania walitumbuiza pia akiwemo pia na Davido kutoka nchini Nigeria.
Tazama picha hapo chini:-
|
Vanessa Mdee "Vee Money" |
|
Ommy Dimpoz |
|
Baadhi ya mashabiki waliohudhuria tamasha la Serengeti Fiesta |
|
Banana Zorro |
|
Young Killah |
|
Waje kutoka Nigeria |
|
Victoria Kimani |
|
Rachel na wanenguaji wake |
|
Barnaba akitoa burudani ya aina yake |
|
Mwanamuziki Shaa akikata mauno |
|
Msanii kutoka Weusi Joh Makini nae akitumbuiza |
|
Diamond Platnumz na Ney Wa Mitego wakitumbuiza pamoja |
|
Msanii Davido kutoka nchini Nigeria akifanya yake stejini |
Picha: Josephat Lukaza
Labels: Burudani, Events